11 Afya na Magonjwa
Le service de santé mu Danemark
GP yako
Wakati una jiandikisha mu registre national mu muji yenye
unaikala ndani, unaweza chagua GP yenye unapenda; kwa
mufano unaweza sema kama unapendelea kukua na docteur
mwanaume ao mwanamuke.
Moyen ya kutunziwa na l'état inawezekana mu njia ya GP
wako. GP wako anaweza tunza malali zimoya zimoya mara
moya, lakini magonjwa zingine zinaomba spécialiste,
ao lazima ya kuenda ku hôspital mukubwa juu utunziwe
muzuri.
Wakati uko na maumivu mingi ya meno, hauhitaji kuenda
ona GP wako, lakini unaweza enda ku hôpital maramoya
kama inaombwa ukuwe hôspitaliser.
Carte ya assurance malade mu Danemark
Carte yako yenye unatumiwa na mukubwa wa baraza ya
muji yako ni kitambulisho cha kuonesha kama unaweza
kuenda kutunziwa na kupata dawa mu hôpital ya l'état.
Carte yenyewe inaandikiwa ako jina yako, adresse yako, na
numéro ya identification personnelle, na jina pamoya na
adresse ya GP wako.
Beba carte yako ya assurance maladie wakati unasafiri mu Bulaya
Unapashwa kuwa na carte yako wakati unaenda ona daktari
wa meno, wakati kuko ugonjwa ya haraka ao wakati unakuwa
hôspitalisé mu hôpital juu ya ugonjwa fulani. Unapashwa
kubeba carte yako saa yenye unasafiri kuenda inje ya
Danemark. Assurance maladie ina ku couvrir kama unakuwa
mogonjwa, ao unafanya accident wakati uko na tembea
mu Bulaya na uko inje ya Danemark mu siku za kidogo ya
chini ya mwezi moya. Ukitaka kujua mingi, angaliya ku site
ya internet: www.sundhed.dk.
Kuenda ona GP wako mu Danmark ni bure
Kuenda onana na GP wako mu Danemark ni bure kama vile
kukuwa hôspitaliser nayo iko bure. Ni pesa ya kodi yenye
unalipa l'état njoo yenye analipaka ma dawa na ma dépenses
ya ma hôpitaux.
Bitu byenye unapashwa jilipia
Unapashwa kuji nunulia dawa yenye munganga alikuandikia,
unapashwa kulipa bakikutunza meno, bakikutunza maungo
kama vile massage. Lakini inawezekana upate usaidizi kutoka
kwa l'état ku hii matunzo.
Kuona munganga
Kupanga rendez-vous ya kuonana
Ukitaka kuonana na munganga, umupigie simu mbele
kusudi musikilizane wakati na saa zenye munaweza onana.
Ba GP biko na saa za kazi, kuanza saa mbili mpaka saa kumi
ya mangaribi. Atakupatia siku ya kuonana yenye haita pitisha
siku tano kutokea saa yenye ulimuita; na kama hali yako
iko mubaya, ao uko mugonjwa sana anaweza kukuona ile
ile siku.
Vipimo, kutunziwa ao kukutuma ku munganga mwengine
Munganga atakupima na kuona kama atafanya nini. Anaweza kukuandikia dawa.
Munganga anaweza kukutuma kufanya bingine bipimo
(examen) ao unatunziwa na mutu mwengine, kwa mufano
anaweza kutuma kwa munganga wa ngozi ao munganga
wa ba mamans, kwa gynécologue. Kuenda ona specialiste
ni bure, hauta lipa kitu. Munganga wako anaweza kutuma
kwake juu akutunze lakini unaweza lipa tu makuta kidogo ya
dawa. Hii inaweza kuwa kutunziwa na munganga wa kutunza
maungu ao kwa psychologue.
Kwa mwisho, munganga wako anaweza tayarisha mambo yako na kuku hôspiataliser kama ni ya lazima.
Mwenye kutafsiri ao intérprète
Munganga wako anapashwa hakikisha kama uko na sikia
kila kitu. Kama hamuzungumuze luga moya, munganga
anapashwa ita mwenye anaweza ku interprèter. Unaweza
pata maelezo ingine mu chapitre 4, Nouveau citoyen au
Danemark.

Kutembelea ao kuenda ona GP wako
Problèmes psychologiques
"Dépression"
Mu Danemark magonjwa ya kichwa iko kawaida. Kufikiri fikiri
na kuwaza waza maneno yenye inaleta wasi wasi, haiku sawa
vile na kukuwa mugonjwa wa akili. Batu mingi mu Danemark
banatafutaka mutu wakubasaidia na kubatunza juu ya ma
problèmes psychologiques. Kama ulifika Danemark juu ya
kukimbia vita ao umeteswa na batu bengine, hii inaweza
kuacha mutu anakuwa na teseka mu hakili na kichwa yako
haiwezi kutumika sawa sawa.
Magonjwa ya kichwa inaweza leta maumivu ya mwili
Enda onana na munganga wako kama uko na shida ya kichwa
na unataka kusaidiwa. Shida ya kichwa, ya akili na mafikiri
mingi zinaweza kuleta vile mwili kuluma. Kwa mufano, kama
uko na teseka na mugongo, maumivu ya tumbu ao kichwa
yenye haitokane na kitu, ao uko nalala mubaya, inaomba
kuenda onana na munganga wako. Munganga wako
atakupima kuona kama unaweza kuwa na ugonjwa yenye
inatokana na ugonjwa wa kichwa ao na akili yako.
Uliza juu ya shida yako
Munganga wako atakuuliza kama uko na ogopa ao uko
na maneno mingi mu akili yako. Ao kama uko na shida ya
bunyumba yako, ao unakumbuka sana jamaa yako na inchi
yako yenye ulitoka amo. Ao tena, kama ulipita mu maneno
ya kuogopesha sawa ya vita na kuteswa ao tena ya kufungiwa
mu prison.
Munganga wako anapashwa kuchunga sécret yako
Munganga wako anapashwa kuchunga sécret yako, ni
kusema kama hauna risques yoyote ya kumuelezeya
problèmes zako kwa sababu hauwezi kutosha maneno yako
inje. Kyenye unamuambia hawezi kukiambia mutu mwengine
ata kama ni mukubwa wa namuna gani. Lakini kama weye
njoo unamuambia aende ambia mutu ao mukubwa fulani,
ule tu njoo anaweza enda ambiya.
Conseils pyschologiques
Munganga wako anaweza ona kama kukutunza na dawa
peke haiwezi kukusaidia. Anaweza kutuma kwa mwenye
ata kusaidia na ma mashauri, ni mutu mwenye amesoma
saikolojia (psychologie) ya batu.
Kama uko na machungu makali ya kichwa ao ya akili, kwa
juu ya vita ao ya mateso yenye ulipitaka amo, munganga
wako atakutuma fasi kwenye banasaidiaka batu benye biko
na shida hiyo mu kambi ya bakimbizi.
Batoto vile banaweza kuonekana mu hali ya ugonjwa wa akili
Inafaa kujua kama batoto banaweza kuteseka na ugonjwa
wa akili na kuhitaji kusaidiwa. Unaweza kuelezea vile vile
munganga wako, banganga benye banatembeleyanaka,
baalimu benye banafundishaka batoto ku masomo ya batoto.
Banaweza kukuelezea namuna ya weye ya kufanya.
Kazi ya munganga wakati ya hatari
Kuonana na munganga mu saha zenye haziko za kazi
Kama unataka ona munganga kiisha saa kumi mu masiku za
kazi, saa sita za muchana siku ya wikendi ao siku za congés,
unapashwa kumupigiya simu munganga wa urgence. Numéro
yabo iko mu kitabu ya ma adresse za simu, ao ku adresse ya
internet: www.sundhed.dk.
Maulizo
Wakati unaita munganga wa urgence, atakuuliza kama uko najisikia
namuna gani. Ao kama uko namuita juu ya mutu mwengine,
atakuuliza kama ule mutu iko nasikia namuna gani. Anaweza uliza
kama uko na moto na kama ni ya mingi kiasi gani. Atauliza vile vile
kama uko na sikia maumivu wapi. Na kama ulilumia ataku uliza
kama kidonda ni kya pata gani.
Kufatana na majibu yenye umejibu, munganga ataona kama
inafaa uende onana na munganga wako kesho, ao aende kwako
kukuona, ao kama unaweza kujifikisha kwa munganga wa urgence
wa pembeni ya kwako. Bata kuuliza vile vile numero ya kitambulisho
yako, ao ya ule mwenye unaitia munganga kama haiku weye njoo
uko mugonjwa.
Unaweza kuita munganga wa wakati ya magonjwa ya hatari na ya gafla kama ni lazima sana.
Unaweza kuita munganga wa wakati ya hatari na gafla wakati
inaomba kumukimbilia; apana kumuita ovyo ovyo na saa zote,
yeye haiku munganga wa kutunza wakati ugonjwa iko ya kawaida
tena na mu masaa za kazi za kawaida, lakini kama hauone sawa
unaweza muita.
Wakati wa hali ya hatari 112, urgence
Mu hali ya hatari
Kama mutu anaanguka na kukosa ufahaamu, kama hawezi
kupumua, kama anafanya ajali, unapashwa pigia banganga ya hali
ya hatari, numéro yabo ni 112.
Pale ku centre ya urgence kwenye umepigia simu, bata kuuliza jina
yako, numéro ya téléphone yako na kwenye uko. Sasa banaweza
kutumia gari ya bagonjwa ao polisi, ao musaada wa hali yeyote
itatumiwa mara moya.
Kupimisha batoto na kubapatia vaccin
Ma éxamens kenda
Kuanza ku âge ya posho tano mpaka miaka 15, mutoto
wako ata pimiwa na muganga mara kenda juu ya afya yake.
Bipimo saba bya kwanza, bitakuwa mbele aanze kuenda ku
masomo, na byengine bipimo mbili wakati ameingia na
kumaliza masomo.
Programme ya examination
Kupima batoto inafataka programme. But ya kubapima ni
kuhakikisha kama batoto wamesaidiwa mu hali yabo ya kuishi
muzuri. Mu hii hali, weye na munganga wako munaweza
kuona kama mutoto iko na shida gani na ku amua kumusaidia
kama inahitajika.
Fanya rendez-vous juu ya saa ya kuonana
Unapashwa sikilizana na munganga wako juu ya zile vipimo
saba za mutoto kama itakua siku gani.
Vaccinations kwa bure
Mutoto anaweza kuchanjwa ku magonjwa mingi. Vaccinations
ziko za bure. Ni munganga wako njoo anachanjaka mutoto
wako. Hii inaweza kuwa mu saa yenye mutoto iko na tunziwa
kwa kawaida.
Ni ba authorités ba santé bamu Danemark njoo banaonaka
kama batoto banaweza kuwa vacciner juu ya kupiganisha
malali gani na wakati gani. Haya magonjwa ni: kidonda ya koo
(Di), Tetanos (Te), Kikohozi ya kelele (Ki), Polio (Pol), Suluba,
Suluba ya kijermani (MFR), na Meningite (Hib).
Suluba ya kijerumani
Suluba ya kijermani ikipata mama wakati ya mamba iko na
hatari ya kufanya mototo azaliwe na kilema fulani. Sababu ya
hii wewe mwanamuke unapashwa kupata chanjo ya kuzuwiya
hiyo mbele ya kupata mimba kama hauya pataka ile saluba
ao kama hauya pataka chanjo ya hii suluba.
Batoto ya Danmark banapataka chanjo kufatana na program hii:| Miaka | Chanjo |
| Myezi mitatu | Di-Te-Ki-Pol-Hib |
| Myezi mitano | Di-Te-Ki-Pol-Hib |
| Myezi kumi na mbili | Di-Te-Ki-Pol-Hib |
| Myezi kumi na tano | MFR I |
| Miaka tano | Di-Te-Ki-Pol |
| Miaka kumi na mbili | MFR II |
Chanjo zengine
Kama uko mama ya mutoto na uko na ugonjwa ya maini
kuvimba, mutoto atachanjwa kusudi asipate ile ugonjwa.
Mutoto atachanjiwa mara moya akisha zaliwa. Mutoto
ataanza zingine chanjo akifikisha posho ine mpaka posho
tano, myezi mbili, na mu myezi kumi na mbili.
Kama mutu moya wa mu jamaa alishaka pata ile ugonjwa ya
maini kuvimba, batu bengine bote bamu jamaa ile batapata
ile chanjo ku bure na GP wako.
Chanjo mbele ya kusafiri
Kama unahitaji chanjo mbele ya kuenda safari, utalipa makuta juu uipate.
Sema na uulize
Afya muzuri na magonjwa ni bitu binaonekana
na ni vie privée ya mutu. En même temps tuna
elewa ugonjwa mu namuna mbali mbali kufatana
na culture yenye tulikomaliyaka ndani. Kwa sababu
hii, kutokuelewana inaweza kutokeya kama cultures
za tafauti zinakutanana na namuna ya kuelewa
mambo ya afya ya mutu. Spéciallement inakuwaka
ngufu kusikilizana.
Batu benye banatumika ku hôpital batakuambia juu
ya matunzo yako, haki zako na devoirs zako kama
mugonjwa. Inafaa usikilize muzuri maneno yenye
bata kuambia, na ku bitii, na byenye batakuambia
inafaa ubifanye. Lakini ni muzuri vile ubaambiye
kama bitu gani unataka bakufanyiye kwa wakati uko
mugonjwa, na kuuliza kama hauelewe kitu.
Ku hospitalini
Kupimiwa na kutunziwa
Unaweza kukuwa hôspitalisé kama umelumia ao umekuwa
mugonjwa. Ao tena unaweza kutumwa na munganga wako
juu ufanye ma examens médicaux ao utunziwa ku hôpital.
Ma examens za mingi na kutunziwa binaweza kuwa mbele
ya weye ukuwe hôspitalisé. Hii ina kuruhusu kutunziwa na
kurudia ku nyumba kwa ile siku.
Choix libre ya hôpital
Kufatana na kutunziwa, unaweza chagua hôpital yenye
unapenda ukuwe hôspitalisé ndani. Kama unachagua
hospitali ya mu région yenye hauishi ndani, inaweza
kuwa nguvu kupata kitanda, na inaweza acha usikuwe
ata hospitalisé. Elezea muganga wako juu ya kuchagua
hospitali.
Chumba ya bagonjwa mingi
Kama unapanga mu hospitali, mutakua mu chumba na
bagonjwa bengine bawili ao batatu. Banaume na banamuke
banapangaka mu ma chumba mbalimbali.
Sheria za chakula na saa za kuona bagonjwa
Usalama na kimya
Bagonjwa banatakaka kimya na usalama. Hii njoo maana
hospitali mingi ziko na saa zakuona amo bagonjwa. Na
benye banakuya ona bagonjwa lazima basifanye fuyo na
baheshimiye bagonjwa bote.
Hospitali inatayarishaka chakula, nguo na fasi ya kunawia
Hôpital inajikazaka kufanya bitu byote juu ya bagonjwa
bakule, bavale nguo yenye iko muzuri, na babatimizie byenye
banapenda. Benye banakuya ona bagonjwa banaweza kuya
tu na matunda, ao na chakula kama bamesikilizana na benye
banatumika ku hôpital na kuchunga wagonjwa wabo.
Batoto mu hospitali
Bazazi banaweza lala na batoto mu hospital
Ma hôpitaux mingi zinatayarishaka fasi ya bazazi benye
biko na batoto bagonjwa . Bazazi ya batoto bana bakiaka
ku hôspitali na mu masaa zenye haziko zaku tembeleya
amo bagonjwa.
Hospitali za kutunza bagonjwa ya kichwa na akili (hôpital psychiatrique)
Interviews na kutunziwa kwa dawa
Bagonjwa ba kichwa na akili banaweza kuwa hôspitalisés
mupaka siku batakuwa muzuri. Aba bagonjwa banaweza
eleza juu ya malali yabo na kupata dawa. Mara mingi
bagonjwa banasaidiaka sana wakati ya kutunziwa kwabo. Ma
hôpitaux mingi za bagonjwa cha kichwa na akili, mugonjwa
anaweza pangishiwa mu chumba yake yeye peke yake. Hizi
ma hôpitaux ziko na machumba za kufunguliwa na zenye
zinafungiwaka.
Hospitalisation forcée
Bagonjwa ba kichwa na akili na benye ba na présenter
danger kwabo benyewe na ku batu bengine, banapashwa
pangishiwa mu chumba moya katika izi hôpital. Kama
mugonjwa anakatala atalazimishwa sababu ya hali
yake kama munganga anaona kama hii iko ya lazima.
Hospitalisation forcée ya mugonjwa inakuwaka tuu hivi:
mugonjwa bana mupelekaka mu chumba ya kufungiwa.
Kutunza meno
Kutunza meno ya batoto
Kutunziwa meno kwa bure kotokeya
mwaka ya kuanza mpaka myaka 18
Batoto bote ba mu Danemark banatunziwaka magonjwa ya
meno bure kutokeya myaka yao ya kwanza mpaka banapata
myaka kumi na nane. Banakuwaka naenda ku contrôle
régulièrement. Kule ku ma cliniques banabafundishaka
namuna ya kutunza meno yabo, na kama biko na shida
banatunzwa tuu bure.
Kutunza meno ya mu butoto
Mutoto yako batamuambia akue naenda kuonana na
munganga wa meno mbele afikisha miaka mbili. Ata kama
mutoto hana magonjwa ya meno, ni muzuri tu akuwe
naenda onana na munganga wake wa meno. Ata kama
meno ya mutoto wako zitatokaka mu butoto, unapashwa
tuu kuendelea ku zichunga wakati mutoto angali nazo
mu kinywa yake. Kama haufanye vile, unaweza kuharibisha
meno ya mutoto zenye zitakujaka nyuma ya pale, meno
za bukubwa.
Ma zones mingi ziko na ma cliniques ya meno zenye
zinatumikaka na masomo za batoto. Fasi ingine, wakubwa
wa baraza ya mugine banakuwaka na masikilizano pamoja na
ba baganga ba meno ba kipekee. Lakini tu batoto habawezi
lipa kuonana naye ao kujitunzisha meno kwabo.
Kutunza meno ku masomo
Wakati mutoto wako anaanza masomo batamupeleka kwanza
kupimiwa meno yake. Banganga ba meno banakuyaka ku
mamasomo na kufundisha batoto namuna ya kutunza
meno yabo.
Ni muzuri bazazi kupeleka batoto yabo kuona munganga
wa meno wakati watoto bangali badogo badogo. Kama
itaomba kutunza mutoto meno yake zaidi sana kushinda ile ya
kawaida, baganga batamuuliza kwanza muzazi wa mutoto.
Kutunziwa meno kwa batu bakubwa
Pata munganga wako wa meno wa kipekee
Batu bazima banapashwa enda kujitunzisha meno yabo
na kujilipia benyewe kuanzia ku myaka 18. Kwa kupata
munganga wa meno, unaweza kuangalia mu kitabu ya
ma namba za téléphone. Unapashwa jilipia contrôle na
kutunziwa meno yako, lakini l'état inalipiaka mutu nusu
kidogo. Zenye l'état anakulipiaka zinatoshewaka mara moya
ku facture yenye utalipa.
Kama uko na assurance yako, inaweza kukulipia ile reste ya
facture yenye ungelipa.
Enda ona munganga wako wa meno
Ni muzuri kukuwa na enda ona munganga wako wa meno
kila mara, apana tu wakati iko naluma. Munganga wako
wa meno anaweza ona kashimo mu meno yako ata kama
hakaya anza kuluma. Kutunziwa haitakuwa ya bei kali kama
sawa vile ungelikuya na meno yenye ilikua naluma, na
tena haitakamata ma saa murefu. Inaomba kusikilizana na
munganga wako wa meno namuna ya kukuwa na kuya ku
contrôle ya meno.
Musikilizane saa za kuonana
Unapashwa sikilizana na muganga wako wa meno ma siku ya weye kukuya ku contrôle ya meno, na ma saa ya kufika kwa zile masiku zenye mulisikilizanaka. Kama unataka kukuwa na kuya ku controle, munganga wako atakukumbusha siku yenye utakuyako tena kwa kukutumiya carte postale.
Matunzo ya meno ya batu bagonjwa ya kichwa na akili na vilema fulani fulani
L'état inatayarishaka namuna ya kulipiya aba batu bagonjwa
ya kichwa na akili na vilema fulani fulani juu watunziwe meno.
L'état inalipaka makuta yote yenye banabakatiyaka kulipa.
Kutunzisha meno inje ya saa za kazi
Kama unakuwa na shida ya meno inje ya saa za kazi unaweza
kimbia kuona banganga haba ba urgence ku centre yabo
ya urgence 24 heures sur 24. Juu ubapate, unaweza angalia
mu kitabu ya ma numéros za téléphone.
Dawa
Ukikuwa ao kama hauna ordonnance
Kuko dawa za kununua bila ruhusa ya munganga
(ordonnance), na zengine lazima ukuye na ordonnance kwa
benye banauzishaka madawa. Zengine madawa zinaombaka
tu munganga njoo akuandikie nazo njo batakuuzishiya
azo mu duka ya madawa. Dawa za ivi haziwezi kuwa mu
maduka za kawaida. Ma dawa za kichwa kuluma, za kusaidia
bavutayi kuacha kuvuta, zinaweza kuuziwa mu ma duka ya
kawaida kama vile ku ma supermarchés, na ku ma stations
ya essence.
Dawa za misaada
L'état inaweza kukupatia musaada juu ya kuuza madawa fulani
fulani. Hii musaada inafatanaka na mali na uwezo ya pesa ya
mutu, na quantité ya madawa yenye unatumiya kwa mwaka
nzima. Umulize munganga wako ao mutu waku uzisha
madawa juu ya iyi musaada kwa kutoka kwa l'état.
Chakula muzuri ya afya na kufanya mazoezi (exercice)
Faida ya kuchunga mwili
Mwili inataka vitamine na nguvu kusudi ifanye kazi. Kukula
chakula ya muzuri ni kukula matunda mingi, ma mboga
mboga mingi, na kutumiya sukari na mafuta kidogo.
Kutembeya kidogo na kufanya mazoezi iko ya lazima sana
kwa mwili, na inasaidia ku epuka magonjwa mbali mbali
za masiku izi.
Malali ya diabète, malali ya roho na cancer
Malali kama diabete, tension, malali ya roho na cancer ni
malali za maisha sababu zinatokana na namuna tunaishi.
Leo tuko na viombo byakufanya kazi ya nguvu yenye zamani
tulikuwa nafanya na mikono yetu. Batu mingi biko na makazi yenye banakuaka na ikala muchana muzima yote, kuenda
kwa gari kazini na kurudia kwa gari kutoka kazini. Batu
bengine bakisha choka habapendake kupiga chakula, bana
nunuaka byenye binaisha ivya.
Ni hatari
Chakula zenye ziko na mafuta mingi, sukari mingi,
kutokufanya sport, kuvuta cigarette na kukunywa pombe
mingi inaongezaka hatari ya kupata zile malali zenye
tumetaya hapa yulu. Wakati ingine kama bazazi yako biko
na zile malali, unaweza vile kuzipata. Njoo maana inaomba
ukule chakula cha afia nzuri na kufanya sport.
Ma conseils muzuri juu ya santé
Unaweza kujikaza kupunguza hatari ya kupata ile malali za
hali ya maisha. Ni kusema usivute cigarettes, ukunywe pombe
kidogo na kula chakula ya aina munane, zenye mukubwa
wa afya anaonesha hapa:
Kula matunda na ma legume mingi:
au moins 600 grammes ku siku
Kama unakula grame miasita ya matunda na mboga kwu
siku, utapunguza hatari ya kupata zile malali. Ukikula orange,
bitika na carrote kila siku na unaongeza legume juu unaweza
kufikiya kukula 600 grams. Kalanga na matunda ya kukauka
zinaweza vile kuwa muzuri.
Kula samaki na vitu yote ya kutokana
na samaki mara mingi kwa posho
Samaki ni chakula muzuri ku afya sababu iko na mafuta,
vitamine D na selenium. Karibu chakula zote zinakuaka na izi
bitu. Unaweza kwa mufano kula samaki ya mu kopo, samaki
kwa jina la makrel ama tuna.
Kula viazi, mchele, couscous ao pastakila siku
Mkati, ngano na muchele ni muzuri na ziko na mafuta
kidogo. Chakula zote za mbegu, mikati ni za muzuri sababu
ziko na fibre na vitamin B. Chagua mukati yenye iko na sukari
kidogo, apana ya mweupe sababu inakosa vitu vingine.
Kula sukari kidogo mu chai na
vinywaji vingine na gateau
Sukari iko na nguvu mingi lakini vitu kidogo tu yenye mwili
inahitaji. Sukari mingi inazuwiya nafasi ya kutiya chakula
ya afya.
Kula mafuta kodogo - nyama na
vitu vya kutokana na maziwa
Mwili yako inaomba mafuta lakini kidogo. Ni muzuri kutumia
mafuta ya mimea kuliko ya nyama. Chagua nyama yenye
haina mafuta mingi, maziwa yenye haina mafuta mingi, na
yougourt na frômage yenye haina mafuta mingi.
Kula chakula mbali mbali - na uchunge
kilo zenye zinakustahili
Kula mikati tafauti, matunda, legume, nyama na chakula za
maziwa kila siku. Hizi zita kupatia vitamine zote zenye mwili
yako inaomba. Kama mwili yako inaongezeka, kula kidogo
kidogo na ufanya mazoezi zaidi. Ni raisi kuchunga ma kilo
zako kama uko na fanya mazoezi.
Tumia mai saa uko na kiu
Mwili yako inahitaji karibu litre moya na nusu ya mai kwa siku. Mai ya ku robinet iko muzuri sababu haiko moto.
Fanyisha mwili yako kazi - karibu
ata dakika 30 kwa siku
Panda ku mingazi, tembea, mwili yako inaomba tu dakika 30
kwa siku ya mazoezi. Batoto banaweza fanya ata saa moya ya
mazoezi. Ni muzuri kufanya mazoezi kila siku juu ya kuchunga
kilo zako. Kila modèle ya mazoezi iko ya lazima ku santé ya
batoto, ba jeunes, na kwa batu bakubwa. Mazoezi iko vizuri
ku mwili yako na ku disposition générale ya mwili yako, na
inakusaidiya kuchunga poids idéal yako.
Unaweza kuangaliya ku internet:www.altomkost.dk/ ao www.helse.dk/ kama unataka kujua mingi
Vitu vya kusaidia afya
Vitamine D
Kama uko na ngozi mweusi usikuwe na kosa kutoka inje
sana na utumie vitamine D yenye l'état inatayarisha kwa
kuchunga ngozi yako vizuri. Mwili inatengenezaka vitamine
yake wakati inaota jua inje. Kama mwili yako inakosa ile
nafasi, lazima utumie vitamine D. Uliza muuzishaji wa dawa
akusaidie kupata vitamine D. Batoto wachanga na wadogo
lazima wapewe matoni ya vitamine D. Omba usaidizi kwa
mutumisha wa santé mwenye anakujaga kukutembeleya.
Mwili unatoa vitamine D yake wakati mtu anapigwa na jua.
Alakini ukikuwa ndani ya mu nyumba ao kwenye kivuli,
mwili wako utapata shida kutoa vitamine D, na ni vyakula
chache njoo vinao kuwa na vitamine D. Ikiwa mwili wako
hauna vitamine D ya kutosha, unaweza kupata maumivu
kwenye mikono na miguu na kuhisi kukosa nguvu kwenye
ma muscles zako.
Calcium
Kama haukunyake maziwa mingi ao kukula vitu mingi vya
maziwa, itaomba unapata calcium ya kukusaidia kama vile
500-1000 grams kwa siku.